Monday, June 25, 2012

RONALDO AVUNJA REKODI YA MABAO URENO

Cristiano Ronaldo

Mshambuliaji nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo sasa amefikia rekodi ya muda wote ya upachikaji mabao iliyowekwa na wachezaji wa Ureno katika fainali za Euro. 

Ronaldo amekwea kileleni mwa wafungaji wa kihistoria wa Ureno katika fainali za Euro, akiwa sambamba na Nuno Gomes. 

Hivi sasa, Ronaldo pia ni miongoni mwa wafungaji walio kileleni katika fainali za Euro 2012 baada ya kupachika mabao matatu na kuipeleka Ureno katika hatua ya nusu fainali, sawa na Mario Gomez wa Ujerumani iliyofika pia nusu fainali na Alan Dzagoev na Mario Mandzukic ambao timu zao zimeshatolewa.

No comments:

Post a Comment